斯瓦希里语吧 关注:319贴子:1,227
  • 0回复贴,共1

啊啊啊啊啊

只看楼主收藏回复

"Je utakubali kuolewa na mimi?"
Mwanamme Akamuuliza mpenzi wake ambae ni mtarajiwa wake katika ndoa.
Mwanamke akainua kinywa chake kutaka kuzungumza lakini mwanaume akamzuia na kumwambia yafuatayo;
Akamwambia kabla hujanipa jibu lako, naomba uelewe kabisa ni nini nachokimaanisha na nini haswa kipo katika mahusiano ya ndoa.
Niwe mkweli kwako;
Ninakuomba uje kuwa mke wangu wa ndoa, katika Ndoa mapenzi huwa ni daraja jingine kabisa maana huko kuna nafasi nyingi zaidi za kuonesha upendo kati yetu.
Nitakufanya kama malkia wangu, nitakupenda siku zote, na utakuwa kipaumbele changu.
Mwanaume akamshika mkono mwanamke wake na kuendelea kumwambia, "Lakini unapaswa kutambua kwamba katikati ya ndoa yetu kutakua na misuguano na mikwaruzano ya hapa na pale, mimi sio mkamilifu asilimia 100.
Ninaweza nikakuudhi mara kadhaa, ninaweza kukusababishia hasira, haijalishi ni kiasi gani nitakukosea naomba tu utambue kuwa kukusoma na kukuelewa wewe ni somo endelevu.
Mimi na wewe tumekutana ukubwani, tumelelewa katika familia tofauti. Lazima tu nitakuwa na baadhi ya vitu usivyovipenda. Nivumilie!
Ndio maana siku zote namuomba Mungu azidi kunifunza kukupenda wewe!
Mwanamke akamtizama mwanaume wake kwa macho ya upendo!
Mwanaume akaendela, "vitu vingi sana utavitarajia kwangu nikiwa kama mume wako. Nitakuwa kichwa cha nyumba, nitahitajika kutunza familia na kuiongoza vema, lakini lazima kutakuwa na siku njema na mbaya.
Katika siku mbaya, nifariji, nipe moyo, niamini mimi, nikumbatie na uwe nguzo yangu. Nitafute pale nitakapopotea, nisamehe pale nitakapokosea.
Lakini kama unaona nakuomba vitu vingi basi usikubali kuolewa na mimi. Nataka niwe mkweli kwako kabla hatujaingia katika Ndoa.


1楼2016-03-24 16:28回复